Published On Premiered Sep 26, 2024
LYRICS
Mtoto Iddi kazua balaa
Kijana Iddi kazua mikosi
Mtoto Iddi kazua balaa
Kijana Iddi kazua mikosi
Yuko kama kapandwa na kichaaa
Anahitaji kurekebishwa
Yuko kama kapandwa na kichaaa
Anahitaji kurekebishwa
Kuvumilia Iddi anavyofanya
Inategemea mtu na mtu
Kabila ama kabila
Kuna wengine hawana masihara
Watamletea matatizo asijue wapi pakukimbilia
Watakuletea matatizo usijue wapi pakukimbilia
Iddi zake michapo na pamba za kuazima
Nyumbani ye hakai wanaishi ka makima
Wazazi waliomzaa Iddi anawakosea heshima
Akirudi nyumbani Iddi ananukia pombe
Akiulizwa ametoka wapi anasema dingi usikonde
Na kabla hajaondoka anamkata dingi makonde
Anavyofanya Iddi amerithi kwa baba yake
Sa umleavyo Iddi baba hivyo sio
Atakuja kukamatwa na kesi za mauaji
Iddi ukimtazama ni mtoto wa makamo
Vibaka wamekamatwa ye mwenyewe akiwemo
Wamemfikisha kwa baba yake kasema simo
Wamempiga mapanga kujifanya much know
Anaunguruma na kesi ya kumdhulumu Mr Joseph Kusaga
Hivi sasa anatafutwa alilipe lile deni alilokopa kwa bwana Joe
Ana kesi za wizi zipatazo ishirini na sita
Alivyo na bahati mbaya akikwapua tu wanamshika
Wazazi mpaka mwenyewe ndio ****
Amepoteza nafasi ya kuishi kama Soldier
Kwani Iddi hawezi kula ugali bila mboga
Kutwa nzima Iddi anakaa kizembe wamemroga
Na tena kuna tetesi wanga wamekula kiboga
We Iddi kuwa makini tabia yako haifai
Utapondwa na marungu uone dunia ka hafai
We ni shahidi ni shahidi
Mtoto Iddi kazua balaa
Kijana Iddi kazua mikosi
Mtoto Iddi kazua balaa
Kijana Iddi kazua mikosi
Yuko kama kapandwa na kichaaa
Anahitaji kurekebishwa
Yuko kama kapandwa na kichaaa
Anahitaji kurekebishwa
Kuvumilia Iddi anavyofanya
Inategemea mtu na mtu
Kabila ama kabila
Kuna wengine hawana masihara
Watamletea matatizo asijue wapi pakukimbilia
Watakuletea matatizo usijue wapi pakukimbilia
Iddi ni kijana mwenye sura ya kibandidu
Iddi ni mtoto wa kwanza wa mzee Hamidu
Ukisema tumseme we ni kama umemuadhibu
Huyu Iddi ana laana
Kutumwa kwake ni kama umemuonea
Mkimuachia upenyo mnamkuta amepotea
Haoni raha kuishi ye na yake familia
Katoka na pombe zake tu akirudi ye analia
Anamlilia nani na pombe kanywa mwenyewe
Na huo ni ushauri alioupata kwenye vijiwe
Mzee Hamidu ana dharau kusema lolote liwe
Alianza tu kidogo ye kubadilisha bia
Mtu mzima yupo bar anazitiririsha bia
Anasubiri wateja walewe aweze kuwaibia
Kamatwa kila wiki watu wameshatega njia
Watu wamechukia nini kinachofatia
Ni kumponda na kumuua au Mungu kumuokoa
Huyu Iddi ana laana
Iddi matatani hawezi kupenya dirishani
Wala haishi kwa raha amemuibia na Majani
YeKila siku kesi tu haziishi mahakamani
Asikutane na msamaha
Pita pita kona naona kundi la watu
Wanambeba Iddi kaiba viatu vya watu
Nauliza eti kisa kauza viatu vya watu
Bila mwenyewe kujua kama Iddi amechukua
Song Writer:
Juma Kassim Ally
/ sir_nature
Audio produced & mixed by:
P-Funk Majani
/ majani187
Video directed by:
Numz Visualz
/ director_numz